Abedi Shaona [AFR]
Shaona Abedi   Congo, the Democratic Republic of the
 
 
Mke:
Mume wangu tafadhali, nakuuliza suala
Nijulishe bilikuli, usinifiche mahala
Maana mimi jahili, ujinga wanitawala
Siasa ya Ujamaa, hasa mana (maana) yake nini?

Hasa mana yake nini, Siasa ya Ujamaa
Unambie (uniambie) kwa makini, yapate kunielea
Nami yakae moyoni, roho ipate tulia
Siasa ya Ujamaa, hasa mana yake nini?

Mume:
Ahsante mke wangu, neno lako la maana
Najibu bila uchungu, ujue kila namna
Ama akujali Mungu, Rabi Mola Subhana
Siasa ya Ujamaa, binadamu wote sawa.

Milima haikutani, lakini binadamu hukutana.


:pcars: :F12015Racecar: :F1fuel: :F12015Trophy:
Currently Offline
1 game ban on record | Info
1820 day(s) since last ban
Favorite Group
AfricanForce - Public Group
29
Members
0
In-Game
2
Online
3
In Chat
Uhuru Safari ndefu si rahisi kufikia.
Yazidi robo karne, tangu Uhuru kupata
Watu hainehaine, madaraka tumepata
Shida dhiki tuachane, nazo huko tulopita (tulikopita?)
Uhuru safari ndefu si rahisi kufika.

Tumetaka huru tuwe, kivitendo na fikira
Tusibebe tena mawe, kazi bila ya ajira
Yoyote aheshimiwe, hata akiwa ♥♥♥♥♥♥
Uhuru safari ndefu si rahisi kufikia.

Hayo basi huyapati, bila kufunga safari
Na bora ujizatiti, kuzunguuka sayari (kuzunguka)
Ukibaki umeketi, mambo hayawi shuari
Uhuru safari ndefu si rahisi kufikia.

Mwanzo wa msafara, ni wengi waloshiriki (walioshiriki)
Si kuleta mashikhara, la kutaka ushabiki
Wakafanya makafara, ili Mungu abariki
Uhuru safari ndefu si rahisi kufikia.

Ni safari ngumu sana, hii tuliyoifunga
Mana (Maana) njiaye si pana, tena ni hafifu mwanga
Kwayo budi kushikana, mbeleni tusiyeyonga
Uhuru safari ndefu si rahisi kufikia.

Siku ziliendelea, jahazi hilo latweka!
Dharuba ikatokea, bahari imechafuka
Yapasa kuogelea, hadi mkondo kuvuka
Uhuru safari ndefu si rahisi kufikia.

Wengi walisema wazi, dharuba ilipotokea,
"Hatupandi tena ngazi, jahazini elekea
Ni hatari ilowazi (ililowazi), japo tena laelea"
Uhuru safari ndefu si rahisi kufikia.

Wakarudi kule nyuma, kufuata bwana zao
Wakasema wamekoma, wakabusu nyayo zao
Wale makombo kwa uma, pasipo na mila zao
Uhuru safari ndefu si rahisi kufika.

Watu hawa inafaa, usukani kutopewa
Hawatakata rufaa, umma ukidhulumiwa
Wepesi kuleta baa, kitu wakiahidiwa
Uhuru safari ndefu si rahisi kufika.

Na wale wenye elimu, yako mengi sana mambo
Kuyajua yalazimu, waziwazi bila fumbo
Kitu bora ukarimu, na hasa siku za mwambo
Uhuru safari ndefu si rahisi kufika.

Elimu isiwe fimbo, wanyonge kuwachapia
Elimu isiwe chambo, cha kunasia rupia
Elimu siwe (isiwe) urembo, wanana macho tupia
Uhuru safari ndefu si rahisi kufikia.

Elimu iwe ni mwanga, wanyonge kuangazia
Waondokane na janga, mateso pasi pazia
Kwa wote iwe ni kinga, wabaya kunyamazia
Uhuru safari ndefu si rahisi kufikia.

Ndugu mnaoshiriki, kwenye hii halaiki
Wakati umenidhiki, yabidi niudiriki
Nakuageni Bunduki, hilo jina langu haki
Uhuru safari ndefu si rahisi kufkia.

- Bundiki Chihungi

:F12015Racecar: :F12015Trophy: :F12016Car: :F12016RaceGrid: :F12015Crown: :F1fuel: :F1flag: :F1graph: :F1wreath: :pcars: :repairs:
unclebenzd 12 Dec, 2017 @ 5:53am 
+rep
3477 4 Aug, 2017 @ 11:03pm 
Siku njema huonekana asubuhi.
Squizy' 14 Dec, 2015 @ 6:25am 
.
Jonny Hatse 13 Dec, 2015 @ 2:20pm 
"Ich bin ein Racer, kein Gewinner."
Abedi Shaona nach dem Rennen in Ungarn :^)
Jonny Hatse 13 Dec, 2015 @ 2:17pm 
"Ich bin ja nicht schwul."
Abedi Shaona zur Frage, ob er gelegentlich mit seinem Teamkollegen HansK zu Abend esse. :^)
Jonny Hatse 13 Dec, 2015 @ 2:16pm 
"Mein Vater kommt aus dem Kongo. Er hat also immer eine Knarre in der Hosentasche."
Abedi Shaona sinniert über seine familiären Wurzeln :^)